Du er ikke logget ind
Beskrivelse
SAFARI YANGU ni riwaya ya Kiswahili inayoyateka na kuyaakisi maisha ya vijana wengi wanaotamani kufanikiwa maishani kwa njia ya mkato. Mwandishi amejaribu kutumia ufundi wa lugha kwa kuimulika jamii yake na kuyaibua mambo yanayowasibu vijana wengi wa sasa. Zaharani anatamani kuishi Ulaya akiamini kuwa huko ndiko kwenye pepo ya dunia. Anajenga mazoea na mgeni wa kizungu (Eliza) aliyekuja kijijini kwao kwa ajili ya utafiti wa mambo ya misitu na vyanzo vya maji. Eliza anaamua kugharamia safari ya Zaharani ili aishi Ulaya. Hali tete inamkabili Zaharani baada ya mchumba wa Eliza kubaini kuwa Eliza ndiye aliyeidhamini safari ile. Anaamua kuiwekea mguu safari yake na hapo Eliza anamtelekeza Zaharani hotelini nchini Kenya bila ya matakwa yake. Hamu na shauku ya kwenda Ulaya inapotea na kumsababishia matatizo mengi maishani mwake. Hatimaye, mambo yakamzunguka na kumgeuka.